Girl Shine ya UN Women imenijengea kujiamini na sasa nasaidia familia yangu- Rachael
Listen now
Description
Mizozo na umaskini wa kupindukia kwenye mazingira ya uhitaji mkubwa wa msaada wa kibinadamu huwaweka wasichana katika hatari kubwa ya kukumbwa na ukatili na kunyanyaswa. Shirika la Umoja wa Mataifa la kushughulikia masuala ya wanawake, UN WOMEN kwa kutambua hilo linatekeleza miradi katika kambi za wakimbizi za Dadaab na Kakuma nchini Kenya ili kuwajengea uwezo wasichana barubaru ili hatimaye waweza kuandaa mustakabali bora wa maisha yao. Girls Shine ni moja ya miradi hiyo kupitia mradi mkubwa wa LEAP unaoungwa mkono na serikali ya Japan tangu mwaka 2018. Wasichana wakimbizi na wenyeji wananufaika na mradi huu na sasa wanapaza sauti kama katika Makala hii iliyoandaliwa na UN Women barani Afrika na kusimuliwa na Thelma Mwadzaya.
More Episodes
Katika mahojiano na Idhaa ya Umoja wa Mataifa, afisa mwandamizi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) anayehusika na masuala ya dharura na mnepo, Rein Paulsen ametahadharisha kuwa hatari ya kutokea baa la njaa nchini Sudan ni halisi na kwa hivyo wakati wa kuchukua hatua ni...
Published 04/22/24
Wakati Mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemorkasia Kongo DRC ikiripoti kuwa na zaidi ya wakimbizi wa ndani 738,000 kwa kipindi cha mwaka huu wa 2024 pekee kutokana na kuongezeka kwa machafuko, Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP limeeleza kuwa na uhitaji wa haraka wa...
Published 04/22/24