Parenting from a distance
Listen now
Description
Jambo la kutafuta kwa ajili ya kuangalia na kuhudumia familia yako ni jambo ambalo halikwepeki kwa mwanaume, tena ikiwa ni mwanaume anaewajibika katika majukumu yake. Lakini, kwenye kutafuta wanaume wengi sana wamejikuta ikiwabidi kwenda kuishi mbali na familia zoo ili waweze kuzihudumia na pia waweze kutimiza ndoto walizonazo juu ya familia zao. Kuishi mbali na familia kunakuja na changamoto nyingi sana ambazo labda jamii haizitambui. Wanaume wengi wanateseka na namna ya kulea watoto wao, lakini pia hata namna ya kuboresha mahusiano na wenzi wao huku wakikabiliana na umbali uliopo kati yao. Philip Changala alihamia Dar es Salaam kutoka Dodoma mwaka 2016, akaacha familia yake Dodoma yenye mtoto mdogo kabisa. Leo hii ameamua kuzungumza na sisi namna maisha ya kuwa mbali na familia, hususani familia changa inavyoweza kuwa na changamoto nyingi sana kwa mwanaume, na namna ambavyo inaweza kuwa chanzo kikubwa cha changamoto ya afya ya akili kwa mwanaume. Nadia anaelezea namna ambavyo mwanaume anaweza akapambana na hali hiyo, lakini pia ni hatua zipi za kuchukua ili kuhakikisha nafasi yako kama baba na kama mume bado inabaki hata kama maisha yamekupeleka mbali na familią yako
More Episodes
This is the Allan Lucky’s story of how he went against all odds to become the man he is today. Born in Songea, to a christian Family, Allan describes his early life as being constrained in the triangle of three main things, church, school and home. From an early age it seemed that this is how...
Published 04/02/24
Published 04/02/24
In this captivating episode, join us as we sit down with Hisia, a remarkable individual whose journey from humble beginnings in Arusha to musical acclaim and entrepreneurial success in Dar es Salaam is nothing short of inspiring. From immersing himself in the world of sales and marketing at...
Published 03/19/24