Yesaya Software Podcast Yesaya R. Athuman
-
- Education
-
Ebwana mambo vipi, jina langu ni Yesaya, kila wiki ninakuletea mfululizo wa vipindi kwa njia ya sauti yaani Podcast. Dhumuni langu ni kukuhabarisha, kukuelimisha na kukuletea mijadala mbalimbali kuhusu Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) na mimi nitajikita zaidi kwenye upande wa mifumo ya kompyuta.
-
Switching/Sticking to Programming Languages
Join the conversation with Yesaya and Anderson to talk about Switching/Sticking to Programming Languages.
-
Andika Ujumbe wa Msaaada Utakaojibiwa na Mtu Mwenye Followers Wengi
Kwenye episode hii nimeeleza kwa kina namna ya kuandika ujumbe wa kuomba msaada kwa mtu mwenye followers wengi. Yawezekana ni programmer au mtu mwenye uzoefu kwenye eneo fulani.
-
Niliyojifunza kwenye #DevFestNairobi na Fursa zilizopo kwa Developers
Nimeandaa mjumuisho wa mambo niliyojifunza kwenye #DevFestNairobi na hamasa niliyopata na hivyo nimeona vyema niweze kukushirikisha wenzetu walipo ili nasi tupate kupiga hatua zaidi.
Ndugu yangu, sikuwahi kujua event ya developers kuwa na wahudhuliaji zaidi ya 3000, vyombo kuletwa na kontena la 40 futi. Yaani nina mengi kukubadilisha mtazamo lakini nikaelewa ndio maana makampuni makubwa ya TEHAMA duniani yana ofisi Kenya.
DevFestDar RSVP: http://zipa.me/devfestdar
Be a Speaker: https://sessionize.com/devfest-dar-es-salaam -
Mambo Matatu (3) Muhimu kwa Wanafunzi wa Mwaka wa Kwanza Chuo
Tunapoelekea kufungua vyuo, nimeona ni vyema kuwapa abc wanafunzi wa mwaka wa kwanza hasa katika kozi za TEHAMA. Nimeweka mambo matatu (3) muhimu ya kuzingatia, unaweza niachia maoni yako kule Twitter @yesayasoftware.
-
Nitumie Browser Gani?
Browser ni software application for retrieving, presenting and traversing information resources on the World Wide Web. Lakini pia inawezesha kucapture au kuinput taarifa ambayo inaweza kurudishwa kwa mfumo unaowasilisha, kisha kuhifadhiwa au kuchakatwa inapohitajika.
-
Usijisikie Vibaya Kugoogle
Hey, Mambo vipi,
Leo tutazungumza kuhusu kugoogle au kutafuta majibu ya changamoto unapokuwa kwenye ujenzi wa mfumo. Je, unajisikia vibaya unapogoogle mambo kwenye mtandao kama programmer unanielewa nikisema Stack Overflow. Lakini je, kugoogle kunakufanya wewe kuwa programmer mbaya?
Nitakueleza kwa uzoefu wangu pamoja na programmers mashuhuri kabisa ninaowafahamu ambao pia wameshare uzoefu wao katika hili. Nitakueleza pia kuna time unagoogle na hutapata kitu lakini kuna mtu unamjua ana uzoefu na sala unalohaingaika nalo, nakumbuka usemi wa waswahili, KUULIZA sio Ujinga.
Hii ni Yesaya Software Podcast episode namba 34.