Gumzo la Wiki Podcast: Kenya si tajiri; Wakenya wamwambia Uhuru
Listen now
Description
Kauli ya Rais Kenyatta kuwa Kenya ni namba sita barani Afrika kwa utajiri imewaghadhabisha Wakenya wanaosema umaskini umekithiri nchini. Kuhusu siasa, Rais Kenyatta anasema wanasiasa viana watashindwa na wazee licha ya mbio zao za kisiasa. Je, sasa ni wazi kuwa Uhur anamuunga mkono Odinga kuwania urais? Je, hatima ya OKA ni gani? Aidha, IEBC imejiondoa katika kamati ya pamoja ya maandalizi ya uchaguzi. Maoni yako ni gani? Wanahabari wetu John Mbuthia wa Nyeri na Moses Kiraise wa Pokot Magharibi wametangamana na wananchi kuhusu masuala haya.
More Episodes
Suala la gharama ya maisha limeendelea kumkosesha Hasla usingizi! Ameamua kutumia mbinu tatu; mbolea ya bei nafuu, serikali na sekta binafsi kuagiza tani elfu miatatu za mbolea na kuagiza mahindi ili kukabili uhaba wa chakula. Atafaulu? Aidha, kuna more goodies kwa mahasla, Rais akipata fedha...
Published 12/17/22
Published 12/17/22
Uteuzi wa makatibu umezua mjadala, wana-Azimio wakilalamika kwamba Rift Valley na Mt.Kenya zimependelewa. Unadhani suala la kimaeneo lilizingatiwa? Aidha, Baba anadai Kinoti anaandamwa na anataka majasusi wa kimataifa kualikwa kushughulikia suala la mauaji ya kiholela. Riggy G naye hataki harufu...
Published 11/05/22