Gumzo la Wiki Podcast: Mudavadi ajiunge na Raila ama Ruto?
Listen now
Description
Mjadala mkali unaendelea kufuatia hatua ya Raila Odinga kuwatafuta marafiki wapya wa kisiasa, hasa kwenye eneo la Magharibi baada ya Mudavadi kusisitiza kwamba hatamuunga mkono tena. Aidha, Ruto anawataka Mudavadi na Wetangula wajiunge naye katika UDA. Si hayo tu, ipo hofu kutokana na kupanda kwa maambukizi ya korona hasa baada ya kugunduliwa kwa Omicron hapa Kenya. Wanahabari wetu John Mbuthia wa Nyeri, Moses Kiraise wa Pokot Magharibi na Martin Ndiema wa Trans Nzoia wameshiriki gumzo na wakazi wa maeneo yao kuhusu masuala haya.
More Episodes
Suala la gharama ya maisha limeendelea kumkosesha Hasla usingizi! Ameamua kutumia mbinu tatu; mbolea ya bei nafuu, serikali na sekta binafsi kuagiza tani elfu miatatu za mbolea na kuagiza mahindi ili kukabili uhaba wa chakula. Atafaulu? Aidha, kuna more goodies kwa mahasla, Rais akipata fedha...
Published 12/17/22
Published 12/17/22
Uteuzi wa makatibu umezua mjadala, wana-Azimio wakilalamika kwamba Rift Valley na Mt.Kenya zimependelewa. Unadhani suala la kimaeneo lilizingatiwa? Aidha, Baba anadai Kinoti anaandamwa na anataka majasusi wa kimataifa kualikwa kushughulikia suala la mauaji ya kiholela. Riggy G naye hataki harufu...
Published 11/05/22