Kitendawili cha idadi kubwa ya wabunge kati ya mirengo ya Raila na Ruto bungeni?
Listen now
Description
Mswada wa Marekebisho ya Sheria za Vyama vya Kisiasa umekuwa kichocheo cha mjadala wiki hii, ambapo wengi wanajiuliza iwapo kufaulu kwake kutakuwa mwanzo wa wanasiasa kuaminiana. Je, iwapo mswada huo utafanywa sheria, tutarajie miungano gani, hasa kati ya nani na nani? Na je, mswada huu umeashiria upande gani kuwa na ubabe bungeni? Aidha, tunaangazia mwaliko wa Ruto kwa kina Mudavadi na Wetangula licha ya kusema hawajaalikwa wala kukutana na yeyote kujadili miungano. Je, kuna karata gani ambayo inachezwa na wanasiasa hawa kuelekea uchaguzi mkuu wa Agosti 9 mwaka huu. Vilevile mjadala kuhusu haja ya wanafunzi kufanyiwa vipimo vya kubaini iwapo wanatumia dawa za kulevya au la kabla ya kurejea shuleni. Je, unafikiri hatua hii itasaidia kudumisha nidhamu shuleni? Wanahabari wetu Faith Kutere wa Eldoret, Bernard Lusigi wa Kakamega na Moses Kiraese wa Pokot Magharibi wameshiriki gumzo na wananchi kuhusu masuala haya.
More Episodes
Suala la gharama ya maisha limeendelea kumkosesha Hasla usingizi! Ameamua kutumia mbinu tatu; mbolea ya bei nafuu, serikali na sekta binafsi kuagiza tani elfu miatatu za mbolea na kuagiza mahindi ili kukabili uhaba wa chakula. Atafaulu? Aidha, kuna more goodies kwa mahasla, Rais akipata fedha...
Published 12/17/22
Published 12/17/22
Uteuzi wa makatibu umezua mjadala, wana-Azimio wakilalamika kwamba Rift Valley na Mt.Kenya zimependelewa. Unadhani suala la kimaeneo lilizingatiwa? Aidha, Baba anadai Kinoti anaandamwa na anataka majasusi wa kimataifa kualikwa kushughulikia suala la mauaji ya kiholela. Riggy G naye hataki harufu...
Published 11/05/22