Gumzo la Wiki Podcast; Mudavadi awazuia Odinga na Ruto kuhudhuria NDC
Listen now
Description
Earthquake aliyoahidi Musalia Mudavadi inasubiriwa kwa hamu kuu Jumapili. Amewaalika wana'OKA na kuwafungia nje Ruto na Raila. Wakenya wana maoni gani? Aidha, cheche baina ya Raila na Ruto zimezidi, kuhusu urushaji mawe na kuitana majina. Haya yanahatarisha utangamano nchini? UDA tayari imeandikia ICC ikidai serikali inafadhili vurugu kwa manufaa ya Raila. Vilevile tunaangazia kesi ya BBI katika Mahakama ya Juu. Je, reggae itarejea? Kadhalika tunazamia suala la mili katika Mto Yala. Wanahabari wetu Moses Kiraese wa Pokot Magharibi, William Omasire wa Nyamira na John Mbuthia wa Nyeri wanatupambia makala haya
More Episodes
Suala la gharama ya maisha limeendelea kumkosesha Hasla usingizi! Ameamua kutumia mbinu tatu; mbolea ya bei nafuu, serikali na sekta binafsi kuagiza tani elfu miatatu za mbolea na kuagiza mahindi ili kukabili uhaba wa chakula. Atafaulu? Aidha, kuna more goodies kwa mahasla, Rais akipata fedha...
Published 12/17/22
Published 12/17/22
Uteuzi wa makatibu umezua mjadala, wana-Azimio wakilalamika kwamba Rift Valley na Mt.Kenya zimependelewa. Unadhani suala la kimaeneo lilizingatiwa? Aidha, Baba anadai Kinoti anaandamwa na anataka majasusi wa kimataifa kualikwa kushughulikia suala la mauaji ya kiholela. Riggy G naye hataki harufu...
Published 11/05/22