Siasa na Gumzo: Jubilee yafufuka? OKA nayo yapata marafiki wapya
Listen now
Description
Baada ya kimya kingi na fukuzafukuza chamani, hatimaye Rais Uhuru Kenyatta amefanya mkutano na viongozi wa Jubilee katika Ikulu. Ikumbukwe chama hicho kimepanga Mkutano wa Kitaifa wa Wajumbe, NDC tarehe 25 Februari, 2022 katika Ukumbi wa KICC, mjadala ukiwa kuwafurusha rasmi Ruto na wandani wake kutoka chama hicho, mpango wa kushirikiana na miungano mingine na kumfanyia kampeni Raila Odinga. Vilevile mjadala mkali umechacha kuhusu mabadiliko ya Sheria za Uchaguzi. Wana-OKA nao baada ya pigo la kondokewa na Musalia Mudavadi na Moses Wetangula imewapata washirika wengine wawili. Je, ni muungano gani una ufuasi makubwa? Kwa masuala na maswali haya, wanahabari wetu Moses Kiraese wa Pokot Magharibi, Faith Kutere wa Uasin Gishu na Martin Ndiema wa Trans Nzoia wamewashirikisha wakazi katika gumzo wiki hii.
More Episodes
Suala la gharama ya maisha limeendelea kumkosesha Hasla usingizi! Ameamua kutumia mbinu tatu; mbolea ya bei nafuu, serikali na sekta binafsi kuagiza tani elfu miatatu za mbolea na kuagiza mahindi ili kukabili uhaba wa chakula. Atafaulu? Aidha, kuna more goodies kwa mahasla, Rais akipata fedha...
Published 12/17/22
Published 12/17/22
Uteuzi wa makatibu umezua mjadala, wana-Azimio wakilalamika kwamba Rift Valley na Mt.Kenya zimependelewa. Unadhani suala la kimaeneo lilizingatiwa? Aidha, Baba anadai Kinoti anaandamwa na anataka majasusi wa kimataifa kualikwa kushughulikia suala la mauaji ya kiholela. Riggy G naye hataki harufu...
Published 11/05/22