Siasa Podcast; Ni kwanini viongozi wengi hasa wawakilishi wadi wametemwa katika michujo za vyama?
Listen now
Description
Mchujo wa vyama vya kisiasa unapoendelea, lipo jambo moja bainifu kuhusu matokeo kuhusu ngome za Naibu wa Rais William Ruto kulinganishwa na ngome ya Raila Odinga. Kwenye eneo la Bonde la Ufa ambako Ruto ana ufuasi mkubwa, baadhi ya wanasiasa wenye tajriba wamelambishwa sakafu huku vijana wengi wakiingia ulingoni. Na huko Nyanza, wanasiasa wengi waliokuwapo uongozini wamedumishwa hasa katika nyadhifa za ubunge, useneta na ugavana. Aidha, katika ngome zote mbili, idadi kubwa ya wawakilishi wadi waliokuwapo wamelambishwa sakafu na wapya kushinda tiketi. Hali hii inamaanisha nini kisiasa? Beatrice Maganga analiangazia suala hili.
More Episodes
Suala la gharama ya maisha limeendelea kumkosesha Hasla usingizi! Ameamua kutumia mbinu tatu; mbolea ya bei nafuu, serikali na sekta binafsi kuagiza tani elfu miatatu za mbolea na kuagiza mahindi ili kukabili uhaba wa chakula. Atafaulu? Aidha, kuna more goodies kwa mahasla, Rais akipata fedha...
Published 12/17/22
Published 12/17/22
Uteuzi wa makatibu umezua mjadala, wana-Azimio wakilalamika kwamba Rift Valley na Mt.Kenya zimependelewa. Unadhani suala la kimaeneo lilizingatiwa? Aidha, Baba anadai Kinoti anaandamwa na anataka majasusi wa kimataifa kualikwa kushughulikia suala la mauaji ya kiholela. Riggy G naye hataki harufu...
Published 11/05/22