Gumzo na Siasa Podcast; Manifesto za Ruto na Wajackoyah
Listen now
Description
Mgombea urais wa UDA, William Ruto amezindua manifesto yake akiangazia nguzo sita; kupunguza gharama ya maisha, kumaliza uhaba wa walimu, matibabu bila malipo, kujenga nyumba elfu 250 kila mwaka, kukuza biashara na kuimarisha kilimo. Ahadi hizi zinatekeleka? Upande mwingine Wajackoyah ameweka wazi manifesto yake akijumuisha mambo ya kiajabu. Mara atahamisha jiji la Nairobi hadi Isiolo, sijui kufuga nyoka, kuvunja sekta ya bodaboda na kuwaajiri wahudumu hao katika mashamba ya bangi na mengine mengi ya kushangaza. Ni manifesto gani ni nzuri? Halafu Kenya Kwanza inasema bandari ya Mombasa imeuzwa huku serikali ikikana. Kadhalika Baba ameanza vita dhidi ya Chebukati. Anasema manual register sharti itumike sambamba na electronic. Chebukati anasema la hasha. Kwa nini Baba anasisitiza ni lazima manual itumike? Haya yanajiri huku suala la zoning likitikisa nyumba ya Baba. Wagombea wasio maarufu wanaambiwa wajiondoe kuwapisha wenye nguvu. Benard Lusigi wa Kakamega, Edwin Mbugua wa Nyeri na Martin Ndiema akiwa Trans Nzoia wanatupambia makala haya.
More Episodes
Suala la gharama ya maisha limeendelea kumkosesha Hasla usingizi! Ameamua kutumia mbinu tatu; mbolea ya bei nafuu, serikali na sekta binafsi kuagiza tani elfu miatatu za mbolea na kuagiza mahindi ili kukabili uhaba wa chakula. Atafaulu? Aidha, kuna more goodies kwa mahasla, Rais akipata fedha...
Published 12/17/22
Published 12/17/22
Uteuzi wa makatibu umezua mjadala, wana-Azimio wakilalamika kwamba Rift Valley na Mt.Kenya zimependelewa. Unadhani suala la kimaeneo lilizingatiwa? Aidha, Baba anadai Kinoti anaandamwa na anataka majasusi wa kimataifa kualikwa kushughulikia suala la mauaji ya kiholela. Riggy G naye hataki harufu...
Published 11/05/22