Gumzo la GMO; Azimio yamkosoa Hasla | Gumzo la Wiki Podcast
Listen now
Description
GMO imezua gumzo, Azimio wakipinga. Kalonzo naye anasema Rais Ruto analenga kuangamiza kilimo cha mimea ya kiasili. Mbali na hayo, unadhani kwamba Kalonzo anatoshea viatu vya Odinga katika upinzani? Baba naye angali anamlaumu Chebukati na mataifa ya kigeni, kwamba yaliingilia uchaguzi wa Kenya! Unasemaje? Si hayo tu, Azimio inasema Ruto amekuwa kiguu na njia, bila kwanza kutimiza ahadi kwa Wakenya. Nawe unatathmini vipi utendakazi wa Ruto ndani ya siku 30 tangu kuapishwa? Wanahabari wetu William Omasire wa Nyamira, Edwin Mbugua wa Nyeri, Clinton Ambujo wa Kisumu na Martin Ndiema wa Trans Nzoia wanasema na wananchi.
More Episodes
Suala la gharama ya maisha limeendelea kumkosesha Hasla usingizi! Ameamua kutumia mbinu tatu; mbolea ya bei nafuu, serikali na sekta binafsi kuagiza tani elfu miatatu za mbolea na kuagiza mahindi ili kukabili uhaba wa chakula. Atafaulu? Aidha, kuna more goodies kwa mahasla, Rais akipata fedha...
Published 12/17/22
Published 12/17/22
Uteuzi wa makatibu umezua mjadala, wana-Azimio wakilalamika kwamba Rift Valley na Mt.Kenya zimependelewa. Unadhani suala la kimaeneo lilizingatiwa? Aidha, Baba anadai Kinoti anaandamwa na anataka majasusi wa kimataifa kualikwa kushughulikia suala la mauaji ya kiholela. Riggy G naye hataki harufu...
Published 11/05/22