GUMZO LA WIKI PODCAST; Uhuru asema atamuunga mgombea wa NASA; hoja za Wakenya
Listen now
Description
Suala la viongozi wote kutakiwa kuwa na digrii ili kuwania nafasi mbalimbali za kisiasa limezua gumzo nchini huku Naibu wa Rais, William Ruto akiungana na wanaopinga hitaji hilo lililotajwa na IEBC. Tayari Seneta Kipchumba Murkomen ameandaa mswada unaolenga kufutilia mbali hitaji hilo huku watakaowania wakitakiwa kuwa na uwezo wa kusoma na kuandika lugha za Kiswahili na Kiingereza pekee na wenye mahitaji maalumu kujua lugha ya ishara. Je, uongozi unategemea kiwango cha masomo? Aidha, Rais Kenyatta amesema yu tayari kumuunga mkono mgombea wa NASA suala ambalo limempandisha hasira Ruto. Isitoshe, Kalonzo ameapa kutokuwa mgombea mwenza wa Raila, huku akiambiwa aache kubweka. Wanahabari wetu, John Mbuthia wa Nyeri na Moses Kiraese wa Pokot Magharibi wamewashirikisha Wakenya katika gumzo. hili.
More Episodes
Suala la gharama ya maisha limeendelea kumkosesha Hasla usingizi! Ameamua kutumia mbinu tatu; mbolea ya bei nafuu, serikali na sekta binafsi kuagiza tani elfu miatatu za mbolea na kuagiza mahindi ili kukabili uhaba wa chakula. Atafaulu? Aidha, kuna more goodies kwa mahasla, Rais akipata fedha...
Published 12/17/22
Published 12/17/22
Uteuzi wa makatibu umezua mjadala, wana-Azimio wakilalamika kwamba Rift Valley na Mt.Kenya zimependelewa. Unadhani suala la kimaeneo lilizingatiwa? Aidha, Baba anadai Kinoti anaandamwa na anataka majasusi wa kimataifa kualikwa kushughulikia suala la mauaji ya kiholela. Riggy G naye hataki harufu...
Published 11/05/22