UNICEF inasisitiza umuhimu wa kucheza katika ukuaji wa watoto
Listen now
Description
Shirika la Umoja wa Mataifa shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF inasisitiza mchango muhimu wa kucheza katika ukuaji wa watoto na afya yao ya akili. Makala hii inatupeleka Nairobi Kenya kwa mwandishi wetu Thelma Mwadzaya aliyekuwa shuhuda wa maadhimisho ya kwanza ya siku ya kucheza duniani yaliyofayika wiki hii katika moja ya shule ya msingi inayofadhiliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF nchini humo katika kampeni maalum ya kudumisha michezo kwa watoto hasa mashuleni.
More Episodes
Nchini Tanzania, Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) linaendesha programu ya mafunzo yanayolenga kuboresha ujuzi wa wataalamu wa mifugo katika kudhibiti magonjwa ya wanyama na kuimarisha afya ya mifugo ili kuihakikishia jamii uhakika wa chakula na chakula salama. John Kabambala...
Published 06/25/24
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayotupeleka nchini Tanzania kumulikaza juhudi za  kuimarisha afya ya mifugo ili kuihakikishia jamii uhakika wa chakula na chakula salama. Pia tunakuletea muhutasari wa habari zikiwemo za Gaza, mabaharia, na ripoti ya ya matumizi ya pombe. Mashinani...
Published 06/25/24