Description
Mara nyingi Ubalozi unapotangaza fursa mpya ya soko- swali linaloulizwa na watu wengi ambao wanafikiria kuchangamkia fursa hiyo ni "wananunua kwa bei gani au offer yao ni kiasi gani". Ni vizuri kuwa na ufahamu wa jumla kuhusu mwenendo wa bei ya soko la dunia la bidhaa hiyo. Hata hivyo ni muhimu zaidi kwa anayetaka kuuza bidhaa - awe ndio mtoa bei kwani mwenye mali ndio anajua gharama aliyoingia kuipata mali yake na ili asipate hasara anatakiwa kuuza kwa bei gani.Hivyo, unapojipanga kuuza bidhaa nje- ni muhumu ukajua bei itakayokupa faida ni ipi.